-
2 Mambo ya Nyakati 22:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Athalia,+ mama ya Ahazia, alipoona kwamba mwanawe amekufa, alitoka na kuangamiza uzao wote wa kifalme* wa nyumba ya Yuda.+ 11 Hata hivyo, Yehoshabeathi binti ya mfalme alimchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia, akamwiba kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliopaswa kuuawa na kumweka yeye pamoja na mlezi wake katika chumba cha ndani cha kulala. Yehoshabeathi binti ya Mfalme Yehoramu+ (alikuwa mke wa kuhani Yehoyada+ na dada ya Ahazia) alifanikiwa kumficha ili Athalia asimwone, kwa hiyo hakumuua.+ 12 Akakaa pamoja nao kwa miaka sita, akiwa amefichwa katika nyumba ya Mungu wa kweli Athalia alipokuwa akiitawala nchi.
-