-
Isaya 38:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
38 Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa karibu afe.+ Nabii Isaya+ mwana wa Amozi akaja na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Wape maagizo watu wa nyumba yako, kwa maana utakufa; hutapona.’”+ 2 Ndipo Hezekia akaugeuza uso wake kuelekea ukutani, akaanza kusali hivi kwa Yehova: 3 “Nakusihi, Ee Yehova, tafadhali, kumbuka+ jinsi ambavyo nimetembea mbele zako kwa uaminifu na kwa moyo kamili,+ nami nimetenda mambo mema machoni pako.” Kisha Hezekia akaanza kulia sana na kububujikwa na machozi.
-