-
Isaya 39:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
39 Wakati huo mfalme wa Babiloni, Merodak-baladani mwana wa Baladani alimtumia Hezekia barua na zawadi,+ kwa maana alisikia kwamba alikuwa mgonjwa na sasa amepona.+ 2 Hezekia akawakaribisha kwa furaha* na kuwaonyesha nyumba yake yenye hazina+—fedha, dhahabu, mafuta ya zeri na mafuta mengine yenye thamani, ghala lake lote la silaha, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hakuna kitu chochote ambacho Hezekia hakuwaonyesha katika nyumba yake mwenyewe* na katika milki yake yote.
-