-
2 Mambo ya Nyakati 33:2-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Alitenda maovu machoni pa Yehova, akafuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.+ 3 Alijenga upya mahali pa juu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amebomoa,+ akajenga madhabahu kwa ajili ya Mabaali na kutengeneza miti mitakatifu,* naye akaliinamia jeshi lote la mbinguni na kuliabudu.+ 4 Alijenga pia madhabahu katika nyumba ya Yehova,+ ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Nitaweka jina langu Yerusalemu milele.”+ 5 Naye alijenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni katika nyua mbili za nyumba ya Yehova.+ 6 Na pia aliwateketeza* motoni wanawe mwenyewe+ katika Bonde la Mwana wa Hinomu;+ alifanya uchawi,+ alifanya uaguzi,* alifanya ulozi, na kuwaweka rasmi watu wanaowasiliana na roho na wabashiri.+ Alitenda kwa kiwango kikubwa sana mambo maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.
-