-
2 Wafalme 21:2-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Manase alitenda maovu machoni pa Yehova, akafuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.+ 3 Alijenga upya mahali pa juu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amebomoa,+ akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali na kutengeneza mti mtakatifu,*+ kama alivyofanya Ahabu mfalme wa Israeli.+ Naye akaliinamia jeshi lote la mbinguni na kuliabudu.+ 4 Alijenga pia madhabahu katika nyumba ya Yehova,+ ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Nitaweka jina langu Yerusalemu.”+ 5 Naye alijenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni+ katika nyua mbili za nyumba ya Yehova.+ 6 Naye alimteketeza* motoni mwana wake mwenyewe; alifanya uchawi, alitafuta ishara za ubashiri,+ na kuwaweka rasmi watu wanaowasiliana na roho na wabashiri.+ Alitenda kwa kiwango kikubwa sana mambo maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.
-