105 Mshukuruni Yehova,+ liitieni jina lake,
Yajulisheni mataifa matendo yake!+
2 Mwimbieni, mwimbieni sifa,
Tafakarini kazi zake zote zinazostaajabisha.+
3 Jivunieni jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+
4 Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake.
Utafuteni uso wake daima.
5 Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,
Miujiza yake na hukumu alizotangaza,+
6 Enyi uzao wa Abrahamu mtumishi wake,+
Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+