8 “Mshukuruni Yehova,+ liitieni jina lake,
Yajulisheni mataifa matendo yake!+
9 Mwimbieni, mwimbieni sifa,+
Tafakarini kazi zake zote zinazostaajabisha.+
10 Jivunieni jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+
11 Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake,
Utafuteni uso wake daima.+
12 Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,+
Miujiza yake na hukumu alizotangaza,
13 Enyi uzao wa Israeli mtumishi wake,+
Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+