Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 16:8-13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “Mshukuruni Yehova,+ liitieni jina lake,

      Yajulisheni mataifa matendo yake!+

      9 Mwimbieni, mwimbieni sifa,*+

      Tafakarini* kazi zake zote zinazostaajabisha.+

      10 Jivunieni jina lake takatifu.+

      Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+

      11 Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake,

      Utafuteni uso* wake daima.+

      12 Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,+

      Miujiza yake na hukumu alizotangaza,

      13 Enyi uzao wa* Israeli mtumishi wake,+

      Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+

  • Zaburi 96:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,

      Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.+

  • Zaburi 145:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Watatangaza utukufu wa ufalme wako+

      Na kusema kuhusu nguvu zako,+

      ל [Lamed]

      12 Ili kuwajulisha wanadamu matendo yako yenye nguvu+

      Na fahari yenye utukufu ya ufalme wako.+

  • Isaya 12:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Na siku hiyo mtasema:

      “Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,

      Yajulisheni mataifa matendo yake!+

      Tangazeni kwamba jina lake limekwezwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki