6 Kisha Daudi akamuuliza hivi Ahimeleki Mhiti+ na Abishai+ mwana wa Seruya,+ ndugu ya Yoabu: “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kwenda kwa Sauli kambini?” Abishai akajibu: “Mimi nitashuka pamoja nawe.”
6 Ndipo Daudi akamwambia Abishai:+ “Huenda Sheba+ mwana wa Bikri atatuletea madhara makubwa zaidi kuliko Absalomu.+ Wachukue watumishi wangu mimi bwana wako umfuatie, ili asipate majiji yenye ngome na kutuponyoka.”
17 Mara moja Abishai+ mwana wa Seruya akaja kumsaidia,+ akampiga Mfilisti huyo na kumuua. Wakati huo wanaume wa Daudi wakamwapia hivi: “Usiende tena vitani pamoja nasi!+ Usiizime taa ya Israeli!”+