Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 22:14-20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Basi kuhani Hilkia, Ahikamu, Akbori, Shafani, na Asaya wakaenda kwa nabii wa kike anayeitwa Hulda.+ Alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi, mtunzaji wa chumba cha mavazi, naye alikuwa akiishi katika Wilaya ya Pili ya Yerusalemu; wakazungumza naye huko.+ 15 Hulda akawaambia, “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Mwambieni hivi mtu aliyewatuma kwangu: 16 “Yehova anasema, ‘Nitaleta msiba mahali hapa na kwa wakaaji wake, maneno yote ya kitabu ambacho mfalme wa Yuda amesoma.+ 17 Kwa sababu wameniacha na wanaifukizia miungu mingine+ moshi wa dhabihu ili kunikasirisha kwa kazi zote za mikono yao,+ ghadhabu yangu itawaka dhidi ya mahali hapa nayo haitazimwa.’”+ 18 Lakini mwambieni hivi mfalme wa Yuda aliyewatuma kutafuta ushauri wa Yehova: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno ambayo umesikia, 19 kwa sababu moyo wako ulikuwa msikivu,* nawe ukajinyenyekeza+ mbele za Yehova uliposikia mambo niliyosema dhidi ya mahali hapa na wakaaji wake—kwamba watakuwa kitu cha kutisha na laana—nawe ukayararua mavazi yako+ na kulia mbele zangu, mimi pia nimekusikia, asema Yehova. 20 Ndiyo sababu nitakuzika pamoja na mababu zako,* nawe utalazwa kwa amani katika kaburi lako, na macho yako hayataona msiba wote nitakaoleta mahali hapa.’”’” Kisha wakampelekea mfalme jibu hilo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki