Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 34:22-28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Basi Hilkia, pamoja na wale waliotumwa na mfalme, wakaenda kwa nabii wa kike aliyeitwa Hulda.+ Alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi, mtunzaji wa chumba cha mavazi, naye alikuwa akiishi katika Wilaya ya Pili ya Yerusalemu; wakazungumza naye huko.+ 23 Akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Mwambieni hivi mtu aliyewatuma kwangu: 24 “Yehova anasema, ‘Nitaleta msiba mahali hapa na kwa wakaaji wake,+ laana zote zilizoandikwa katika kitabu+ walichosoma mbele ya mfalme wa Yuda. 25 Kwa sababu wameniacha+ na wanaifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu ili kunikasirisha+ kwa kazi zote za mikono yao, ghadhabu yangu itamwagika mahali hapa nayo haitazimwa.’”+ 26 Lakini mwambieni hivi mfalme wa Yuda aliyewatuma kutafuta ushauri wa Yehova: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno ambayo umesikia,+ 27 kwa sababu moyo wako ulikuwa msikivu,* nawe ukajinyenyekeza mbele za Mungu uliposikia mambo yake kuhusu mahali hapa na wakaaji wake, ukajinyenyekeza mbele zangu na kuyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, mimi pia nimekusikia,+ asema Yehova. 28 Ndiyo sababu nitakuzika pamoja na mababu zako,* nawe utalazwa kwa amani katika kaburi lako, na macho yako hayataona msiba wote nitakaoleta mahali hapa na kwa wakaaji wake.’”’”+

      Kisha wakampelekea mfalme jibu hilo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki