-
2 Mambo ya Nyakati 34:22-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Basi Hilkia, pamoja na wale waliotumwa na mfalme, wakaenda kwa nabii wa kike aliyeitwa Hulda.+ Alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi, mtunzaji wa chumba cha mavazi, naye alikuwa akiishi katika Wilaya ya Pili ya Yerusalemu; wakazungumza naye huko.+ 23 Akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Mwambieni hivi mtu aliyewatuma kwangu: 24 “Yehova anasema, ‘Nitaleta msiba mahali hapa na kwa wakaaji wake,+ laana zote zilizoandikwa katika kitabu+ walichosoma mbele ya mfalme wa Yuda. 25 Kwa sababu wameniacha+ na wanaifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu ili kunikasirisha+ kwa kazi zote za mikono yao, ghadhabu yangu itamwagika mahali hapa nayo haitazimwa.’”+ 26 Lakini mwambieni hivi mfalme wa Yuda aliyewatuma kutafuta ushauri wa Yehova: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno ambayo umesikia,+ 27 kwa sababu moyo wako ulikuwa msikivu,* nawe ukajinyenyekeza mbele za Mungu uliposikia mambo yake kuhusu mahali hapa na wakaaji wake, ukajinyenyekeza mbele zangu na kuyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, mimi pia nimekusikia,+ asema Yehova. 28 Ndiyo sababu nitakuzika pamoja na mababu zako,* nawe utalazwa kwa amani katika kaburi lako, na macho yako hayataona msiba wote nitakaoleta mahali hapa na kwa wakaaji wake.’”’”+
Kisha wakampelekea mfalme jibu hilo.
-