16 basi, mimi nitawatendea mambo haya: nitawaadhibu kwa taabu, kwa kifua kikuu na homa kali, na kufanya macho yenu yadhoofike na uhai wenu uzorote.* Mtapanda mbegu zenu bure, kwa maana maadui wenu watazila.+
15 “Lakini msipoisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu kwa kuwa waangalifu kutenda amri zake zote na sheria zake ninazowaamuru leo, laana hizi zote zitawajia na kuwatangulia:+
17 “Lakini moyo wenu ukikengeuka+ na kukataa kusikiliza, mshawishiwe na kuiinamia miungu mingine na kuiabudu,+18 nawaambia ninyi leo kwamba hakika mtaangamia.+ Hamtaishi kwa muda mrefu katika nchi mnayovuka Yordani ili kuimiliki.
11 Waisraeli wote wamekiuka Sheria yako na kukuacha kwa kutotii sauti yako, hivi kwamba ukatumwagia laana na kiapo kilichoandikwa katika Sheria ya Musa mtumishi wa Mungu wa kweli,+ kwa maana tumekutendea Wewe dhambi.