-
2 Wafalme 24:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Sedekia alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 11 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 19 Sedekia aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo Yehoyakimu alitenda.+ 20 Mambo hayo yalitukia Yerusalemu na Yuda kwa sababu ya hasira ya Yehova, mpaka alipowatupa mbali kutoka mbele zake.+ Na Sedekia akamwasi mfalme wa Babiloni.+
-
-
Yeremia 52:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
52 Sedekia+ alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 11 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 2 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo Yehoyakimu alitenda.+ 3 Mambo hayo yalitukia Yerusalemu na Yuda kwa sababu ya hasira ya Yehova, mpaka alipowatupa mbali kutoka machoni pake.+ Na Sedekia akamwasi mfalme wa Babiloni.+
-