Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 36:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Sedekia+ alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 11 huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Pia alimwasi Mfalme Nebukadneza,+ aliyekuwa amemwapisha kwa jina la Mungu, akaendelea kuwa mkaidi* na mwenye moyo mgumu na kukataa kumgeukia Yehova Mungu wa Israeli.

  • Yeremia 27:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Pia nilimwambia Mfalme Sedekia+ wa Yuda maneno hayohayo, nikisema: “Wekeni shingo zenu chini ya nira ya mfalme wa Babiloni na mumtumikie yeye na watu wake, nanyi mtaendelea kuishi.+

  • Yeremia 38:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kisha Yeremia akamwambia Sedekia: “Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Ukijisalimisha* kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni, uhai wako utaokoka,* na jiji hili halitateketezwa kwa moto, na wewe na watu wa nyumba yako mtaokoka.+

  • Ezekieli 17:12-15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Tafadhali iambie nyumba ya uasi, ‘Je, hamtambui maana ya mambo haya?’ Sema, ‘Tazama! Mfalme wa Babiloni alikuja Yerusalemu, akamchukua mfalme wake na wakuu wake na kurudi pamoja nao Babiloni.+ 13 Isitoshe, alimchukua mmoja aliyekuwa wa uzao wa*+ kifalme, akafanya naye agano na kumwapisha.+ Kisha akawachukua watu mashuhuri wa nchi,+ 14 ili ufalme huo ushushwe, usiweze kuinuka, ili uendelee kuwapo ikiwa tu utashika agano lake.+ 15 Lakini mwishowe mfalme huyo alimwasi+ kwa kutuma wajumbe wake Misri ili apate farasi+ na jeshi kubwa kutoka huko.+ Je, atafanikiwa? Je, yule anayefanya mambo hayo ataponyoka adhabu? Je, anaweza kuvunja agano na bado aponyoke?’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki