-
Yeremia 22:24, 25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 “‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Yehova, ‘hata kama Konia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, angekuwa pete ya muhuri kwenye mkono wangu wa kuume, ningekung’oa kutoka hapo! 25 Nami nitakutia mkononi mwa wale wanaotaka kukuua,* mkononi mwa wale unaowaogopa, mkononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, na mkononi mwa Wakaldayo.+
-
-
Yeremia 52:31, 32Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Kisha katika mwaka wa 37 tangu Mfalme Yehoyakini+ wa Yuda alipopelekwa uhamishoni, katika mwezi wa 12, siku ya 25 ya mwezi huo, Mfalme Evil-merodaki wa Babiloni, katika mwaka alioanza kutawala, alimwachilia huru Mfalme Yehoyakini wa Yuda na kumtoa gerezani.+ 32 Alizungumza naye kwa fadhili na kukikweza kiti chake cha ufalme juu zaidi kuliko viti vya wafalme wengine waliokuwa pamoja naye Babiloni.
-