Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 24:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Mfalme Yehoyakini wa Yuda akatoka nje kwenda kukutana na mfalme wa Babiloni,+ akiwa pamoja na mama yake, watumishi wake, wakuu wake, na maofisa wa makao yake;+ na mfalme wa Babiloni akamchukua mateka katika mwaka wa nane wa utawala wake.+

  • 2 Wafalme 24:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Basi akampeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ alimpeleka pia mama ya mfalme, wake za mfalme, maofisa wa makao yake, na viongozi wa nchi, akawapeleka uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu.

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka 18 alipoanza kutawala, alitawala kwa miezi mitatu na siku kumi huko Yerusalemu; naye aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova.+ 10 Mwanzoni mwa mwaka,* Mfalme Nebukadneza aliagiza aletwe Babiloni,+ pamoja na vyombo vyenye thamani vya nyumba ya Yehova.+ Akamweka Sedekia ndugu ya baba yake kuwa mfalme wa Yuda na Yerusalemu.+

  • Yeremia 24:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kisha Yehova akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya hekalu la Yehova, baada ya Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kumpeleka uhamishoni Yekonia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, pamoja na wakuu wa Yuda, mafundi, na wahunzi;* aliwatoa Yerusalemu na kuwapeleka Babiloni.+

  • Yeremia 29:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Haya ndiyo maneno ya barua ambayo nabii Yeremia aliwatumia kutoka Yerusalemu wazee waliobaki miongoni mwa watu waliopelekwa uhamishoni, makuhani, manabii, na watu wote, ambao Nebukadneza alikuwa amewatoa Yerusalemu na kuwapeleka uhamishoni Babiloni, 2 baada ya Mfalme Yekonia+ na mama malkia,+ maofisa wa makao ya mfalme, wakuu wa Yuda na Yerusalemu, na mafundi na wahunzi* kuondoka Yerusalemu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki