Yeremia
22 Yehova anasema hivi: “Shuka nyumbani kwa* mfalme wa Yuda, upeleke ujumbe huu. 2 Utasema, ‘Sikia neno la Yehova, ewe mfalme wa Yuda unayeketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi, wewe pamoja na watumishi wako na watu wako, wale wanaoingia kupitia malango haya. 3 Yehova anasema hivi: “Tekelezeni haki na uadilifu. Na mtu anayenyang’anywa, mwokoeni kutoka mikononi mwa mtu laghai. Msimtese mkaaji yeyote mgeni, na msimdhuru yatima yeyote au mjane.+ Nanyi msimwage damu yoyote isiyo na hatia mahali hapa.+ 4 Kwa maana mkijitahidi kufuata neno hili, basi wafalme wanaoketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ wataingia kupitia malango ya nyumba hii, wakiwa wamepanda magari na farasi, wao pamoja na watumishi wao na watu wao.”’+
5 “‘Lakini msipoyatii maneno haya, ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe,’ asema Yehova, ‘kwamba nyumba hii itakuwa ukiwa.’+
6 “Kwa maana Yehova anasema hivi kuhusu nyumba ya mfalme wa Yuda,
‘Wewe ni kama Gileadi kwangu,
Kama kilele cha Lebanoni.
Lakini nitakufanya uwe nyika;
Hakuna jiji lako hata moja litakalokaliwa.+
Wataikata mierezi yako iliyo bora zaidi
Na kuiangusha ndani ya moto.+
8 Na mataifa mengi yatapita kando ya jiji hili na kila mmoja atamwambia mwenzake: “Kwa nini Yehova alilitendea hivi jiji hili kuu?”+ 9 Nao watajibu: “Kwa sababu waliliacha agano la Yehova Mungu wao na kuiinamia miungu mingine na kuitumikia.”’+
10 “Msimlilie aliyekufa,
Na msimsikitikie.
Badala yake, mlilieni sana yule anayeondoka,
Kwa maana hatarudi tena kuiona nchi alimozaliwa.
11 “Kwa maana Yehova anasema hivi kumhusu Shalumu*+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda anayetawala badala ya Yosia+ baba yake, ambaye ameondoka mahali hapa: ‘Hatarudi hapo tena. 12 Kwa maana atakufa mahali walipompeleka uhamishoni, naye hataiona tena nchi hii.’+
13 Ole wake anayejenga nyumba yake bila uadilifu
Na vyumba vyake vya juu bila haki,
Anayemfanya mwanadamu mwenzake amtumikie bure,
Na ambaye anakataa kumlipa malipo yake;+
14 Yule anayesema, ‘Nitajijengea nyumba yenye nafasi kubwa
Yenye vyumba vya juu vyenye nafasi kubwa.
Nitaiwekea madirisha
Nami nitazifunika kuta zake kwa mbao za mierezi na kuipaka rangi nyekundu.’
15 Je, utaendelea kutawala kwa sababu unawashinda wengine kwa kutumia mierezi?
16 Alitetea haki halali ya mwenye kuteseka na maskini,
Basi akafanikiwa.
‘Hiyo ndiyo maana ya kunijua, sivyo?’ asema Yehova.
17 ‘Lakini macho yako na moyo wako unakazia tu faida yako isiyo ya haki,
Kumwaga damu isiyo na hatia,
Na kufanya ulaghai na unyang’anyi.’
18 “Kwa hiyo Yehova anasema hivi kumhusu Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda,
‘Hawatamwombolezea:
“Aa! ndugu yangu! Aa! dada yangu!”
Hawatamwombolezea:
“Aa! Ewe bwana! Aa! mfalme!”
20 Panda mpaka Lebanoni na upaze kilio,
Paza sauti yako huko Bashani.
21 Nilisema nawe ulipokuwa salama.
Lakini ulisema, ‘Sitatii.’+
Hii imekuwa njia yako tangu ujana wako,
Kwa maana hujaitii sauti yangu.+
Kisha utaaibishwa na kufedheheshwa kwa sababu ya msiba wako wote.
Uliye na kiota kati ya mierezi,+
Jinsi utakavyougua uchungu utakapokupata,
24 “‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Yehova, ‘hata kama Konia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, angekuwa pete ya muhuri kwenye mkono wangu wa kuume, ningekung’oa kutoka hapo! 25 Nami nitakutia mkononi mwa wale wanaotaka kukuua,* mkononi mwa wale unaowaogopa, mkononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, na mkononi mwa Wakaldayo.+ 26 Nami nitakutupa wewe pamoja na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine ambako hamkuzaliwa, nanyi mtakufa huko. 27 Nao hawatarudi kamwe katika nchi wanayoitamani.*+
28 Je, mtu huyu Konia ni chungu tu kilichodharauliwa na kuvunjika,
Chombo ambacho hakuna mtu anayekitaka?
Kwa nini yeye na wazao wake wameangushwa chini
Na kutupwa katika nchi wasiyoijua?’+
29 Ewe dunia,* dunia, dunia, sikia neno la Yehova.
30 Yehova anasema hivi: