-
Kumbukumbu la Torati 29:24-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 wao pamoja na mataifa yote watauliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii?+ Ni nini kilichomfanya awake hasira kali hivi?’ 25 Kisha watasema, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano la Yehova,+ Mungu wa mababu zao, ambalo alifanya pamoja nao alipowatoa nchini Misri.+ 26 Lakini walienda na kuabudu miungu mingine na kuiinamia, miungu ambayo hawakuwa wameijua na ambayo hakuwaruhusu waiabudu.*+
-
-
1 Wafalme 9:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Na nyumba hii itakuwa marundo ya magofu.+ Kila mtu atakayepita karibu nayo ataitazama kwa mshangao, atapiga mluzi na kuuliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+ 9 Kisha watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova Mungu wao, aliyewatoa mababu zao kutoka nchini Misri, nao wakashikamana na miungu mingine, wakaiinamia na kuiabudu. Ndiyo sababu Yehova aliwaletea msiba huo wote.’”+
-