-
1 Wafalme 8:46-50Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 “Wakikutendea dhambi (kwa sababu hakuna mwanadamu asiyetenda dhambi),+ nawe uwakasirikie vikali na kuwaacha mikononi mwa maadui, na waliowateka wawapeleke katika nchi ya maadui, mbali au karibu;+ 47 nao warudiwe na ufahamu wakiwa katika nchi ya watu waliowachukua mateka,+ na kukurudia+ na kuomba kibali chako wakisema, ‘Tumetenda dhambi na kukosea; tumetenda uovu,’+ 48 nao wakurudie kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi* yao yote katika nchi ya maadui wao waliowachukua mateka, nao wasali kwako kuelekea nchi yao ambayo uliwapa mababu zao na kuelekea jiji ambalo umelichagua na nyumba ambayo nimejenga kwa ajili ya jina lako,+ 49 basi usikie kutoka mbinguni, makao yako,+ sala yao na ombi lao la kutaka kibali, nawe utekeleze hukumu kwa ajili yao 50 na uwasamehe watu wako ambao wamekutendea dhambi, na kusamehe makosa yote waliyokukosea. Utafanya waliowateka wawahurumie,* nao watawahurumia+
-