-
2 Mambo ya Nyakati 6:36-39Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
36 “Wakikutendea dhambi (kwa sababu hakuna mwanadamu asiyetenda dhambi),+ nawe uwakasirikie vikali na kuwaacha mikononi mwa maadui, na waliowateka wawapeleke katika nchi fulani, mbali au karibu,+ 37 nao warudiwe na ufahamu wakiwa katika nchi ya watu waliowachukua mateka, na kukurudia na kukuomba kibali katika nchi walikopelekwa mateka, wakisema, ‘Tumetenda dhambi na kukosea; tumetenda uovu,’+ 38 nao wakurudie kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi* yao yote katika nchi walikopelekwa mateka,+ nao wasali kwako kuelekea nchi yao ambayo uliwapa mababu zao na kuelekea jiji ambalo umelichagua+ na nyumba ambayo nimejenga kwa ajili ya jina lako, 39 basi usikie kutoka mbinguni, makao yako, sala yao na ombi lao la kutaka kibali, nawe utekeleze hukumu kwa ajili yao+ na uwasamehe watu wako ambao wamekutendea dhambi.
-