Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 “Lakini msipoisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu kwa kuwa waangalifu kutenda amri zake zote na sheria zake ninazowaamuru leo, laana hizi zote zitawajia na kuwatangulia:+

  • Kumbukumbu la Torati 28:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Yehova atawapeleka ninyi na mfalme mliyemchagua awe juu yenu, kwenye taifa ambalo ninyi hamlijui wala mababu zenu hawakulijua,+ na huko mtaabudu miungu mingine, miungu ya miti na ya mawe.+

  • 2 Wafalme 17:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka jiji la Samaria.+ Kisha akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+

  • 2 Wafalme 25:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Mfalme wa Babiloni aliwaua na kuwaangamiza huko Ribla katika nchi ya Hamathi.+ Hivyo watu wa Yuda wakaenda uhamishoni kutoka katika nchi yao.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 6:36-39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 “Wakikutendea dhambi (kwa sababu hakuna mwanadamu asiyetenda dhambi),+ nawe uwakasirikie vikali na kuwaacha mikononi mwa maadui, na waliowateka wawapeleke katika nchi fulani, mbali au karibu,+ 37 nao warudiwe na ufahamu wakiwa katika nchi ya watu waliowachukua mateka, na kukurudia na kukuomba kibali katika nchi walikopelekwa mateka, wakisema, ‘Tumetenda dhambi na kukosea; tumetenda uovu,’+ 38 nao wakurudie kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi* yao yote katika nchi walikopelekwa mateka,+ nao wasali kwako kuelekea nchi yao ambayo uliwapa mababu zao na kuelekea jiji ambalo umelichagua+ na nyumba ambayo nimejenga kwa ajili ya jina lako, 39 basi usikie kutoka mbinguni, makao yako, sala yao na ombi lao la kutaka kibali, nawe utekeleze hukumu kwa ajili yao+ na uwasamehe watu wako ambao wamekutendea dhambi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki