-
1 Wafalme 9:6-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Lakini ikiwa ninyi na wana wenu mtageuka na kuacha kunifuata na kuacha kushika amri zangu na maagizo yangu ambayo nimeweka mbele yenu, nanyi mwende na kuabudu miungu mingine na kuiinamia,+ 7 nitawaondolea mbali Waisraeli kutoka katika nchi ambayo nimewapa,+ na nyumba ambayo nimeitakasa kwa ajili ya jina langu nitaitupilia mbali kutoka mbele za macho yangu,+ na Israeli itakuwa kitu cha kudharauliwa* na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa mataifa yote.+ 8 Na nyumba hii itakuwa marundo ya magofu.+ Kila mtu atakayepita karibu nayo ataitazama kwa mshangao, atapiga mluzi na kuuliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+ 9 Kisha watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova Mungu wao, aliyewatoa mababu zao kutoka nchini Misri, nao wakashikamana na miungu mingine, wakaiinamia na kuiabudu. Ndiyo sababu Yehova aliwaletea msiba huo wote.’”+
-