-
2 Wafalme 23:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Yosia pia aliondoa nyumba zote za ibada zilizokuwa mahali pa juu katika majiji ya Samaria,+ ambazo wafalme wa Israeli walijenga na kumkasirisha Mungu, akazitendea kama alivyozitendea zile zilizokuwa Betheli.+ 20 Basi makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwa mahali hapo akawatoa dhabihu juu ya madhabahu hizo, naye akateketeza mifupa ya wanadamu juu yake.+ Kisha akarudi Yerusalemu.
-