-
2 Mambo ya Nyakati 17:3-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Yehova aliendelea kuwa pamoja na Yehoshafati kwa sababu alitembea katika njia za awali za Daudi babu yake+ naye hakutafuta Mabaali. 4 Kwa maana alimtafuta Mungu wa baba yake+ na kufuata* amri yake wala si mazoea ya Waisraeli.+ 5 Yehova aliendelea kuuimarisha kabisa ufalme mikononi mwake;+ na watu wote wa Yuda wakaendelea kumpa Yehoshafati zawadi, akawa na utajiri na utukufu mwingi.+ 6 Moyo wake ukawa jasiri katika njia za Yehova, na hata aliondoa mahali pa juu+ na miti mitakatifu*+ huko Yuda.
-