-
2 Wafalme 10:10-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Basi jueni kwamba hakuna neno hata moja la Yehova ambalo Yehova amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu litakalokosa kutimia,*+ na Yehova amefanya yale aliyosema kupitia mtumishi wake Eliya.”+ 11 Basi Yehu akawaua watu wote waliobaki wa nyumba ya Ahabu kule Yezreeli, na pia watu wake wote mashuhuri, marafiki zake, na makuhani wake,+ hakumwacha mtu yeyote wa nyumba yake akiwa hai.+
12 Kisha akaondoka na kuelekea Samaria. Njiani kulikuwa na nyumba ya kuwakatia kondoo manyoya. 13 Huko Yehu akakutana na ndugu za Mfalme Ahazia+ wa Yuda, naye akawauliza, “Ninyi ni nani?” Wakasema: “Sisi ni ndugu za Ahazia, nasi tunashuka kwenda kuwajulia hali wana wa mfalme na wana wa mama malkia.” 14 Mara moja akasema: “Wakamateni wakiwa hai!” Basi wakawakamata wanaume 42 wakiwa hai na kuwachinja kando ya tangi la maji la nyumba ya kuwakatia kondoo manyoya. Hakumwacha yeyote kati yao akiwa hai.+
-