Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 21:19-24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Mwambie hivi: ‘Yehova anauliza hivi: “Je, umemuua mtu+ na kuchukua mali yake?”’+ Kisha mwambie, ‘Yehova anasema hivi: “Mahali ambapo mbwa waliramba damu ya Nabothi, ndipo watakapoiramba damu yako mwenyewe.”’”+

      20 Ahabu akamwambia Eliya: “Yaani umenipata, ewe adui yangu?”+ Akajibu: “Nimekupata. ‘Kwa sababu umeazimia* kutenda maovu machoni pa Yehova,+ 21 sasa ninakuletea msiba, nami nitafagia kabisa baada yako na kumwangamiza kila mwanamume* wa Ahabu,+ kutia ndani wasio na uwezo na walio dhaifu katika Israeli.+ 22 Nami nitaifanya nyumba yako iwe kama nyumba ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha+ mwana wa Ahiya, kwa sababu umenikasirisha na kusababisha Waisraeli watende dhambi.’ 23 Pia Yehova anasema hivi kumhusu Yezebeli: ‘Mbwa watamla Yezebeli katika shamba la Yezreeli.+ 24 Mtu yeyote wa Ahabu anayefia jijini mbwa watamla, na yeyote anayefia shambani ndege wa angani watamla.+

  • 2 Wafalme 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Unapaswa kuiangamiza nyumba ya Ahabu bwana wako, nami nitailipizia kisasi damu ya watumishi wangu manabii na watumishi wote wa Yehova ambao Yezebeli aliwaua.*+

  • 2 Wafalme 9:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Waliporudi na kumwambia Yehu, akasema: “Jambo hilo linatimiza neno hili la Yehova+ alilosema kupitia mtumishi wake Eliya, Mtishbi: ‘Katika shamba la Yezreeli, mbwa wataula mwili wa Yezebeli.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki