-
Mambo ya Walawi 13:45, 46Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
45 Mtu mwenye ukoma anapaswa kuvaa mavazi yaliyoraruka, hapaswi kutunza nywele za kichwa chake, naye anapaswa kufunika masharubu yake na kusema hivi kwa sauti: ‘Mimi si safi, mimi si safi!’ 46 Kwa muda wote atakaokuwa na ugonjwa huo hatakuwa safi. Kwa kuwa yeye si safi, ataishi akiwa ametengwa. Ataishi nje ya kambi.+
-
-
Hesabu 12:14, 15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Yehova akamjibu Musa: “Ikiwa baba yake angemtemea mate usoni moja kwa moja, je, hangeaibika kwa siku saba? Acha atengwe nje ya kambi kwa siku saba,+ kisha anaweza kurudishwa kambini.” 15 Kwa hiyo Miriamu akatengwa nje ya kambi kwa siku saba,+ na watu hawakuendelea na safari hadi Miriamu aliporudishwa kambini.
-