-
2 Mambo ya Nyakati 28:5-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Kwa hiyo Yehova Mungu wake akamtia mikononi mwa mfalme wa Siria,+ hivi kwamba wakamshinda, wakachukua mateka wengi, na kuwapeleka Damasko.+ Alitiwa pia mikononi mwa mfalme wa Israeli, ambaye aliwaua watu wake wengi. 6 Kwa maana Peka+ mwana wa Remalia aliwaua watu 120,000 huko Yuda katika siku moja, wote walikuwa wanaume jasiri, kwa sababu Waisraeli walikuwa wamemwacha Yehova Mungu wa mababu zao.+ 7 Na Zikri, shujaa Mwefraimu, alimuua Maaseya mwana wa mfalme na Azrikamu aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme,* na Elkana aliyekuwa wa pili baada ya mfalme. 8 Zaidi ya hayo, Waisraeli waliwachukua mateka ndugu zao 200,000—wanawake, wana, na mabinti; walichukua pia nyara nyingi na kuzipeleka Samaria.+
-