-
1 Mambo ya Nyakati 28:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Alimpa ramani ya kila kitu alichoambiwa kupitia mwongozo wa roho kuhusu ujenzi wa nyua+ za nyumba ya Yehova, vyumba vyote vya kulia chakula vilivyoizunguka, hazina za nyumba ya Mungu wa kweli, na hazina za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu;*+ 13 pia kuhusu vikundi vya makuhani+ na Walawi, kuhusu kazi zote za utumishi wa nyumba ya Yehova, na kuhusu vyombo vyote vya utumishi wa nyumba ya Yehova;
-
-
2 Mambo ya Nyakati 8:14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Pia, alipanga vikundi vya makuhani+ kwa ajili ya utumishi wao kulingana na sheria ya Daudi baba yake, na Walawi katika vituo vyao vya kazi, ili watoe sifa+ na kuhudumu mbele ya makuhani kulingana na utaratibu wa kila siku, na walinzi wa malango katika vikundi vyao kwenye malango mbalimbali,+ kwa maana hivyo ndivyo alivyoamuru Daudi, mtu wa Mungu wa kweli.
-