Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 6:31, 32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Hao ndio watu ambao Daudi aliwaweka ili waongoze uimbaji katika nyumba ya Yehova baada ya Sanduku kuletwa likae* humo.+ 32 Ndio waliokuwa na jukumu la kusimamia uimbaji katika hema la ibada, yaani, hema la mkutano mpaka Sulemani alipoijenga nyumba ya Yehova huko Yerusalemu,+ nao walitekeleza utumishi wao kulingana na maagizo waliyopewa.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 15:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Ndipo Daudi akawaambia wakuu wa Walawi wawaweke ndugu zao waimbaji ili waimbe kwa shangwe na sauti kubwa, kwa ala za muziki: vinanda, vinubi,+ na matoazi.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 16:37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Kisha Daudi akamwacha Asafu+ na ndugu zake hapo mbele ya sanduku la agano la Yehova ili wahudumu daima mbele ya Sanduku+ hilo, kulingana na utaratibu wa kila siku.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 16:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 nao walikuwa pamoja na Hemani+ na Yeduthuni ili wapige tarumbeta, matoazi, na ala zilizotumiwa kumsifu* Mungu wa kweli; na wana wa Yeduthuni+ walikuwa langoni.

  • 1 Mambo ya Nyakati 25:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Isitoshe, Daudi na wakuu wa vikundi vya utumishi waliwatenga baadhi ya wana wa Asafu, Hemani, na Yeduthuni+ ili watoe unabii kwa kutumia vinubi, vinanda,+ na matoazi.+ Hii ndiyo orodha ya wanaume waliowekwa rasmi kwa ajili ya utumishi huo:

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki