Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 7:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Lakini hivi ndivyo mtakavyowatendea: Bomoeni madhabahu zao, vunjeni nguzo zao takatifu,+ kateni miti yao mitakatifu,*+ na kuteketeza sanamu zao za kuchongwa.+

  • 2 Wafalme 18:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea+ mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia+ mwana wa Mfalme Ahazi+ wa Yuda akawa mfalme.

  • 2 Wafalme 18:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Yeye ndiye aliyeondoa mahali pa juu,+ akazivunjavunja nguzo takatifu, na kuukata ule mti mtakatifu.*+ Pia alimpondaponda yule nyoka wa shaba aliyetengenezwa na Musa;+ kwa maana mpaka wakati huo Waisraeli walikuwa wakimfukizia moshi wa dhabihu, na nyoka huyo alikuwa akiitwa sanamu ya nyoka wa shaba.*

  • 2 Mambo ya Nyakati 14:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Asa alitenda yaliyokuwa mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wake. 3 Aliondoa madhabahu za kigeni+ na mahali pa juu, akazivunjavunja nguzo takatifu,+ na kuikata miti mitakatifu.*+

  • 2 Mambo ya Nyakati 34:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Yosia+ alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 31 huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 34:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Katika mwaka wa 8 wa utawala wake, alipokuwa angali mvulana, alianza kumtafuta Mungu wa Daudi babu yake;+ na katika mwaka wa 12, akaanza kusafisha Yuda na Yerusalemu+ kwa kuondoa mahali pa juu+ na miti mitakatifu,* sanamu za kuchongwa,+ na sanamu za chuma.*

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki