-
Nehemia 6:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kisha nikaenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya mwana wa Mehetabeli, alipokuwa amejifungia ndani. Akasema: “Tupange wakati ili tukutane katika nyumba ya Mungu wa kweli, ndani ya hekalu, nasi tufunge milango ya hekalu, kwa maana wanakuja kukuua. Wanakuja kukuua usiku.” 11 Lakini nikasema: “Je, mtu kama mimi anapaswa kukimbia? Je, mtu kama mimi anaweza kuingia hekaluni na aendelee kuishi?+ Sitaingia!” 12 Ndipo nikatambua kwamba Mungu hakuwa amemtuma, bali Tobia na Sanbalati+ walikuwa wamemkodi ili atabiri maneno hayo kunihusu.
-