8Kisha watu wote wakakusanyika wakiwa na kusudi moja katika uwanja wa jiji uliokuwa mbele ya Lango la Maji,+ wakamwambia Ezra+ mwandishi* alete kitabu cha Sheria ya Musa,+ ambayo Yehova alikuwa ameamuru Waisraeli waifuate.+
3 Naye akaisoma kwa sauti kubwa+ katika uwanja wa jiji mbele ya Lango la Maji, kuanzia asubuhi hadi adhuhuri, akawasomea wanaume, wanawake, na wote ambao wangeweza kuelewa; nao watu wakasikiliza kwa makini+ kitabu cha Sheria.