Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Methali 14:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Mwenye hekima hujihadhari na kuepuka uovu,

      Lakini mpumbavu hajali,* naye anajiamini kupita kiasi.

  • Methali 28:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Mwenye furaha ni mtu aliye chonjo sikuzote,*

      Lakini yeyote anayeufanya moyo wake kuwa mgumu ataanguka katika msiba.+

  • Isaya 30:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “Ole wao wana wakaidi,”+ asema Yehova,

      “Wanaotekeleza mipango ambayo si yangu,+

      Wanaofanya miungano,* lakini si kwa roho yangu,

      Ili kuongeza dhambi juu ya dhambi.

  • Danieli 5:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Zaidi alimpa baba yako Nebukadneza ufalme na ukuu na heshima na fahari.+

  • Danieli 5:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Lakini moyo wake ulipokuwa na kiburi na roho yake kuwa ngumu hivi kwamba akatenda kwa kimbelembele,+ alishushwa chini kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, naye akanyang’anywa heshima yake.

  • Zekaria 7:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Waliifanya mioyo yao iwe kama almasi*+ nao walikataa kutii sheria* na maneno ambayo Yehova wa majeshi aliwapa kwa roho yake kupitia manabii wa kale.+ Kwa hiyo Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+

  • Waroma 2:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Lakini kulingana na ukaidi wako na moyo wako usiotubu, unajiwekea akiba ya ghadhabu katika siku ya ghadhabu na ya kufunuliwa kwa hukumu ya uadilifu ya Mungu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki