Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 7:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Lakini makuhani wachawi wa Misri wakafanya jambo hilohilo kwa mazingaombwe yao,+ hivi kwamba moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi, na kama Yehova alivyosema, Farao hakuwasikiliza.+

  • Nehemia 9:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Ingawa uliwaonya ili wairudie Sheria yako, walitenda kwa kimbelembele na kukataa kusikiliza amri zako;+ nao wakatenda dhambi kwa kutofuata masharti yako, ambayo mtu akiyafuata ataishi.+ Lakini walikugeuzia mgongo na kufanya shingo zao ziwe ngumu, nao wakakataa kukusikiliza.

  • Methali 29:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Mtu anayeifanya shingo yake kuwa ngumu baada ya kukaripiwa sana+

      Atavunjwa kwa ghafla, naye hataweza kupona.+

  • Yeremia 16:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Nanyi mmetenda mambo mabaya zaidi kuliko mababu zenu,+ na kila mmoja wenu anaufuata ukaidi wa moyo wake mwovu badala ya kunitii.+ 13 Basi nitawatupa nje ya nchi hii mpaka kwenye nchi ambayo wala ninyi wala mababu zenu hawakuijua,+ na huko mtalazimika kuiabudu miungu mingine mchana na usiku,+ kwa sababu sitawaonyesha kibali.”’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki