-
1 Samweli 2:22-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Sasa Eli alikuwa amezeeka sana, lakini alikuwa amesikia mambo yote ambayo wanawe walikuwa wakiwatendea+ Waisraeli wote na jinsi walivyokuwa wakilala na wanawake waliotumikia kwenye mlango wa hema la mkutano.+ 23 Alikuwa akiwaambia hivi: “Kwa nini mnaendelea kufanya mambo ya aina hii? Kwa maana mambo ninayosikia kuwahusu kutoka kwa watu wote ni mabaya. 24 Msifanye hivyo wanangu, kwa sababu habari ninazosikia zikienea miongoni mwa watu wa Yehova si nzuri. 25 Mwanadamu akimtendea dhambi mwanadamu mwenzake, mtu fulani anaweza kumsihi Yehova kwa niaba yake;* lakini mwanadamu akimtendea dhambi Yehova,+ ni nani anayeweza kusali kwa ajili yake?” Lakini walikataa kumsikiliza baba yao, kwa sababu Yehova alikuwa ameazimia kuwaua.+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.
-