13 Kwa maana uliziumba figo zangu;
Ulinisitiri katika tumbo la mama yangu.+
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia inayoogopesha na kustaajabisha.+
Kazi zako zinastaajabisha,+
Ninajua vizuri sana jambo hilo.
15 Mifupa yangu haikufichwa kwako
Nilipoumbwa sirini,
Nilipofumwa katika sehemu zenye kina za dunia.+
16 Macho yako hata yaliniona nikiwa kiinitete;
Sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chako
Kuhusiana na siku ambazo zingeumbwa,
Kabla sehemu yoyote haijakuwepo.