12 Kisha Yehova akamwambia Shetani: “Tazama! Kila kitu alicho nacho kimo mikononi mwako.* Ila tu usimguse mwanamume huyo!” Kwa hiyo Shetani akaondoka mbele za* Yehova.+
17 Alipokuwa bado anaongea, mwingine akaja na kusema: “Wakaldayo+ walijipanga katika makundi matatu, wakavamia ngamia na kuwachukua, nao wakawaua watumishi kwa upanga. Nimeponyoka mimi peke yangu, nami nimekuletea habari.”