-
Mwanzo 20:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Kisha Mungu wa kweli akamwambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya jambo hili kwa moyo mnyoofu, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee dhambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umguse. 7 Sasa mrudishe mke wa mwanamume huyo, kwa maana mwanamume huyo ni nabii,+ atakuombea dua,+ nawe utaendelea kuishi. Lakini usipomrudisha, ujue kwamba kwa hakika utakufa, wewe na watu wako wote.”
-
-
Mathayo 27:19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Zaidi ya hayo, alipokuwa ameketi kwenye kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe huu: “Mwache mtu huyo mwadilifu, kwa maana niliteseka sana leo katika ndoto kwa sababu yake.”
-