Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 “Ila tu muwe waangalifu na kujihadhari sana, ili msisahau mambo ambayo macho yenu yameona na ili yasiondoke moyoni mwenu siku zote za maisha yenu. Ni lazima pia muwaambie wana wenu na wajukuu wenu.+

  • Kumbukumbu la Torati 6:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Maneno haya ninayokuamuru leo lazima yawe moyoni mwako, 7 nawe lazima uyakazie* kwa wanao+ na kuongea kuyahusu unapoketi nyumbani mwako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.+

  • Kumbukumbu la Torati 6:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 ndipo utakapomwambia mwana wako, ‘Tulikuwa watumwa wa Farao kule Misri, lakini Yehova alitutoa Misri kwa mkono wenye nguvu.

  • Kumbukumbu la Torati 11:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Ni lazima uyakazie maneno haya yangu katika moyo wako na nafsi* yako na kuyafunga kama kumbukumbu kwenye mkono wako, nayo yanapaswa kuwa kama utepe kwenye paji la uso wako.*+ 19 Wafundishe watoto wako maneno haya, na kuongea kuyahusu unapoketi nyumbani mwako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.+

  • Yoshua 4:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 ili yawe ishara kwenu. Ikiwa watoto* wenu watawauliza wakati ujao, ‘Mawe haya ni ya nini?’+ 7 waambieni: ‘Sanduku la agano la Yehova lilipovushwa Yordani, maji ya Yordani yalizuiwa yasitiririke.+ Basi mawe haya yatakuwa kumbukumbu la kudumu kwa Waisraeli.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki