-
Yeremia 7:24-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao;+ badala yake walitembea katika mipango yao* wenyewe, wakifuata kwa ukaidi moyo wao mwovu,+ nao wakarudi nyuma, badala ya kwenda mbele, 25 tangu siku ambayo mababu zenu walitoka nchini Misri mpaka leo hii.+ Basi nikaendelea kuwatuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nilikuwa nikiwatuma kila siku, tena na tena.*+ 26 Lakini walikataa kunisikiliza, nao hawakutega sikio lao.+ Badala yake, walikuwa wakaidi,* nao walitenda mambo mabaya zaidi kuliko mababu zao!
-