Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 2:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Katika siku za mwisho,*

      Mlima wa nyumba ya Yehova

      Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+

      Nao utainuliwa juu ya vilima,

      Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+

       3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:

      “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,

      Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Naye atatufundisha njia zake,

      Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+

  • Zekaria 14:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Na Yehova atakuwa Mfalme juu ya dunia yote.+ Siku hiyo Yehova atakuwa Mungu pekee,+ na jina lake litakuwa ndilo jina pekee.+

  • Ufunuo 7:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Baada ya hapo nikaona, na tazama! umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na jamii na lugha,+ wakiwa wamesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwanakondoo, wakiwa wamevaa kanzu nyeupe;+ na walikuwa na matawi ya mitende mikononi mwao.+ 10 Nao wanaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Wokovu unatoka kwa Mungu wetu, anayeketi kwenye kiti cha ufalme,+ na kwa Mwanakondoo.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki