-
Mika 4:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Mlima wa nyumba ya Yehova+
Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,
Nao utainuliwa juu ya vilima,
Na mataifa yatamiminika kwenye mlima huo.+
2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:
“Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova
Na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Naye atatufundisha njia zake,
Nasi tutatembea katika vijia vyake.”
Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,
Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.
3 Atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifa mengi+
Na kunyoosha* mambo kuhusiana na mataifa yenye nguvu yaliyo mbali.
Watafua panga zao ziwe majembe ya plau
Na mikuki yao iwe miundu.+
Taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine,
Wala hawatajifunza vita tena kamwe.+
-