-
Waamuzi 10:6-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Waisraeli wakaanza tena kutenda maovu machoni pa Yehova,+ nao wakaanza kuabudu Mabaali,+ sanamu za Ashtorethi, miungu ya Aramu,* miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu,+ miungu ya Waamoni,+ na miungu ya Wafilisti.+ Wakamwacha Yehova wala hawakuendelea kumtumikia. 7 Basi hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli, naye akawatia mikononi mwa Wafilisti na Waamoni.+ 8 Kwa hiyo wakawatesa na kuwakandamiza sana Waisraeli mwaka huo—kwa miaka 18 waliwakandamiza Waisraeli wote waliokuwa ng’ambo ya Yordani katika nchi iliyokuwa ya Waamori kule Gileadi.
-