10 Kwa maana kama mvua na theluji inavyomwagika kutoka mbinguni
Nayo hairudi huko mpaka iiloweshe dunia na kuifanya izae na kuchipuka,
Na kumpa mbegu mpandaji na mkate yule anayekula,
11 Hivyo ndivyo neno langu linalotoka katika kinywa changu litakavyokuwa.+
Halitarudi kwangu bila matokeo,+
Bali hakika litatimiza jambo lolote linalonipendeza,+
Na hakika litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma.