Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Ni lazima mzifuate kwa uangalifu,+ kwa sababu watu watakaosikia kuhusu masharti haya yote wataona kwamba mna hekima+ na uelewaji,+ nao watasema, ‘Kwa hakika watu wa taifa hili kubwa wana hekima na uelewaji.’+

  • Yoshua 1:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Ila tu uwe jasiri na imara kabisa, na ufuate kwa uangalifu Sheria yote kama Musa mtumishi wangu alivyokuamuru. Usiende kushoto wala kulia,+ ili utende kwa hekima mahali popote utakapoenda.+ 8 Kitabu hiki cha Sheria kisiondoke kinywani mwako,+ ni lazima ukisome kwa sauti ya chini* mchana na usiku ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo;+ ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.+

  • 1 Wafalme 2:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Ni lazima utimize wajibu wako kwa Yehova Mungu wako kwa kutembea katika njia zake na kushika maagizo yake, amri zake, sheria zake,* na vikumbusho vyake kama vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa;+ ndipo utakapofanikiwa* katika kila jambo unalofanya na kila mahali unapogeuka kwenda.

  • Zaburi 119:100
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 100 Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,

      Kwa sababu ninayatii maagizo yako.

  • 2 Timotheo 3:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Hata hivyo, endelea kufuata mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini,+ ukijua ulijifunza mambo hayo kutoka kwa nani, 15 na kwamba tangu utoto mchanga+ umeyajua maandishi matakatifu,+ ambayo yanaweza kukufanya uwe mwenye hekima ili upate wokovu kupitia imani katika Kristo Yesu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki