Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 4:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Watu kutoka katika mataifa yote walikuja kuisikia hekima ya Sulemani, pamoja na wafalme kutoka kotekote duniani waliokuwa wamesikia kuhusu hekima yake.+

  • 1 Wafalme 10:4-7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Sulemani,+ nyumba aliyojenga,+ 5 chakula kilichokuwa mezani pake,+ jinsi watumishi wake walivyoketi, jinsi watumishi wake walivyohudumu mezani na pia mavazi yao, na wale waliompa vinywaji, na dhabihu zake za kuteketezwa alizotoa kwa ukawaida katika nyumba ya Yehova, alipigwa na bumbuazi.* 6 Basi akamwambia mfalme: “Habari nilizosikia katika nchi yangu kuhusu mafanikio* yako na kuhusu hekima yako zilikuwa za kweli. 7 Lakini sikuamini habari hizo mpaka nilipokuja na kujionea kwa macho yangu mwenyewe. Na kwa kweli sikuwa nimeambiwa hata nusu yake. Hekima yako na ufanisi wako umezidi kwa mbali habari nilizosikia.

  • Danieli 1:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Mfalme alipozungumza nao, hakuna kijana yeyote katika kikundi chote aliyekuwa kama Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria;+ nao wakaendelea kumtumikia mfalme. 20 Katika kila jambo lililohitaji hekima na uelewaji ambalo mfalme aliwauliza, aliona kwamba walikuwa bora mara kumi kuliko makuhani wote wachawi na watu waliofanya mazingaombwe+ katika milki yake yote.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki