21 Yehova hunithawabisha kulingana na uadilifu wangu;+
Hunilipa kulingana na usafi wa mikono yangu.+
22 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,
Nami sijamwacha kwa uovu Mungu wangu.
23 Hukumu zake zote+ ziko mbele yangu;
Sitageuka kando kutoka kwenye sheria zake.+
24 Nitabaki bila lawama+ mbele zake,
Nami nitajiepusha na uovu.+
25 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+
Kulingana na usafi wangu mbele zake.+