-
Yeremia 33:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Nami nitawatakasa kutokana na hatia yote ya dhambi walizonitendea,+ nami nitasamehe hatia yote ya dhambi zao na makosa waliyonikosea.+ 9 Naye atakuwa kwangu jina la furaha, sifa, na uzuri mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia kuhusu wema wote nitakaowapa.+ Nao wataogopa na kutetemeka+ kwa sababu ya wema na amani ninayompa.’”+
-