Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 20:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kisha Mungu wa kweli akamwambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya jambo hili kwa moyo mnyoofu, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee dhambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umguse.

  • Kumbukumbu la Torati 17:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Mtu anayetenda kwa kimbelembele kwa kukataa kumsikiliza kuhani anayemhudumia Yehova Mungu wenu au kukataa kumsikiliza mwamuzi ni lazima afe.+ Ni lazima mwondoe uovu katika Israeli.+

  • 1 Samweli 15:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 kwa maana uasi+ ni sawa na dhambi ya uaguzi,*+ na kutenda kwa kimbelembele ni sawa na kutumia nguvu za uchawi na ibada ya sanamu.* Kwa kuwa umelikataa neno la Yehova,+ yeye pia amekukataa usiwe mfalme.”+

  • 2 Samweli 6:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Uza, na Mungu wa kweli akamuua+ papo hapo kwa sababu ya tendo lake lisilo la heshima,+ akafa hapo karibu na Sanduku la Mungu wa kweli.

  • 2 Mambo ya Nyakati 26:16-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Hata hivyo, mara tu alipokuwa na nguvu, moyo wake ukawa na kiburi ambacho kilisababisha aangamie, naye alikosa kutenda kwa uaminifu kumwelekea Yehova Mungu wake kwa kuwa aliingia katika hekalu la Yehova ili kufukiza uvumba kwenye madhabahu ya uvumba.+ 17 Mara moja kuhani Azaria na makuhani wengine 80 wa Yehova wenye ujasiri wakamfuata humo. 18 Wakamkabili Mfalme Uzia na kumwambia: “Si vyema kwako, Uzia, kumfukizia Yehova uvumba!+ Ni makuhani tu wanaopaswa kufukiza uvumba, kwa maana wao ni wazao wa Haruni,+ waliotakaswa. Toka mahali patakatifu, kwa maana hujatenda kwa uaminifu, na kwa sababu hiyo hutapokea utukufu wowote kutoka kwa Yehova Mungu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki