Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 6:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 “Sasa hizi ndizo amri, masharti, na sheria ambazo Yehova Mungu wako ametoa ili ufundishwe, ili uzishike unapovuka kuingia katika nchi ambayo utaimiliki, 2 ili umwogope Yehova Mungu wako na kushika sheria zake zote na amri zake ambazo ninakuamuru wewe—wewe na mwana wako na mjukuu wako+—siku zote za maisha yako, ili uishi muda mrefu.+

  • Kumbukumbu la Torati 30:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Nachukua mbingu na dunia kuwa mashahidi dhidi yenu leo kwamba nimeweka uzima na kifo mbele yenu, baraka na laana;+ nanyi lazima mchague uzima ili mwendelee kuishi,+ ninyi na wazao wenu,+ 20 kwa kumpenda Yehova Mungu wenu,+ kwa kuisikiliza sauti yake, na kushikamana naye,+ kwa maana yeye ni uzima wenu na kwa uwezo wake mtaishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo Yehova aliapa kwamba angewapa mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo.”+

  • 1 Petro 3:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana “yeyote anayependa uzima na kuona siku zilizo njema, lazima aulinde ulimi wake usiseme mabaya+ na midomo yake isiseme udanganyifu. 11 Na aache mabaya,+ atende mema;+ na atafute amani na kuifuatilia.+ 12 Kwa maana macho ya Yehova* yanawatazama waadilifu, na masikio yake yanasikiliza dua yao,+ lakini uso wa Yehova* uko dhidi ya wale wanaotenda maovu.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki