-
Kumbukumbu la Torati 6:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 “Sasa hizi ndizo amri, masharti, na sheria ambazo Yehova Mungu wako ametoa ili ufundishwe, ili uzishike unapovuka kuingia katika nchi ambayo utaimiliki, 2 ili umwogope Yehova Mungu wako na kushika sheria zake zote na amri zake ambazo ninakuamuru wewe—wewe na mwana wako na mjukuu wako+—siku zote za maisha yako, ili uishi muda mrefu.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 30:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Nachukua mbingu na dunia kuwa mashahidi dhidi yenu leo kwamba nimeweka uzima na kifo mbele yenu, baraka na laana;+ nanyi lazima mchague uzima ili mwendelee kuishi,+ ninyi na wazao wenu,+ 20 kwa kumpenda Yehova Mungu wenu,+ kwa kuisikiliza sauti yake, na kushikamana naye,+ kwa maana yeye ni uzima wenu na kwa uwezo wake mtaishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo Yehova aliapa kwamba angewapa mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo.”+
-
-
1 Petro 3:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kwa maana “yeyote anayependa uzima na kuona siku zilizo njema, lazima aulinde ulimi wake usiseme mabaya+ na midomo yake isiseme udanganyifu. 11 Na aache mabaya,+ atende mema;+ na atafute amani na kuifuatilia.+ 12 Kwa maana macho ya Yehova* yanawatazama waadilifu, na masikio yake yanasikiliza dua yao,+ lakini uso wa Yehova* uko dhidi ya wale wanaotenda maovu.”+
-