30 Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu,+
Karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na busara.
31 Niliona limejaa magugu;
Ardhi ilifunikwa na miiba,
Na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.+
32 Nilitazama hilo na kulitia moyoni;
Nililiona na kujifunza somo hili:
33 Lala kidogo, sinzia kidogo,
Kunja mikono kidogo ili upumzike,
34 Na umaskini wako utakuja kama jambazi,
Na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+