Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Methali 13:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Kuna vitu anavyotamani sana mtu mvivu, ingawa hana chochote,+

      Lakini mwenye bidii atatoshelezwa kikamili.*+

  • Methali 20:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Mvivu halimi katika majira ya baridi kali,

      Kwa hiyo atakuwa akiombaomba wakati wa mavuno, wakati hana chochote.*+

  • Methali 24:30-34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu,+

      Karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na busara.*

      31 Niliona limejaa magugu;

      Ardhi ilifunikwa na miiba,

      Na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.+

      32 Nilitazama hilo na kulitia moyoni;

      Nililiona na kujifunza somo hili:*

      33 Lala kidogo, sinzia kidogo,

      Kunja mikono kidogo ili upumzike,

      34 Na umaskini wako utakuja kama jambazi,

      Na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki